TRUMP APANIA KUMALIZA UHALIFU MAREKANI.
Mgombea urais wa chama cha
Republican nchini Marekani Donald Trump ameahidi kumaliza uhalifu na
ghasia nchini Marekani iwapo atachaguliwa kuwa rais kwenye uchaguzi mkuu
mwezi Novemba.
Aidha, ameahidi kuchukua hatua kali kukabiliana na wahamiaji haramu na akaonga kuwa kwa sasa wahamiaji wanaruhusiwa kuingia na kuishi katika jamii za Marekani bila kuzingatia usalama wa umma.
- Wanawe Trump wafana kongamano la Republican
- Mambo 20 makuu anayoamini Donald Trump
Mfanyabiashara huyo tajiri kutoka Marekani amesema atakomesha sera ya kujenga mataifa na kufanikisha mageuzi ya serikali katika nchi nyingine ambayo amesema imefeli.
Amesema sera hiyo ndiyo chanzo cha matatizo yanayoshuhudiwa nchini Iraq, Libya, Misri na Syria.
- Trump anafanana na Hitler, Rais wa Mexico asema
Ameituhumu Uchina kwa wizi wa haki miliki za Wamarekani, na kuieleza Beijing kama taifa lililohadaa zaidi katika thamani ya sarafu yake katika historia.
Bw Trump ameahidi kushauriana upya na washirika kuhusu mikataba ya kibiashara kuhakikisha Marekani inafaidi
Post a Comment