Header Ads

AKATWA KICHWA NA KUTELEKEZWA KICHAKANI

Mtu mmoja amefariki dunia kwa kukatwa kichwa na kiwiliwili chake kutelekezwa kichakani katika Kijiji cha Rushwa, Kata ya Mushabago, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.


Mwenyekiti wa Kitongoji cha Buyango, Gasper Joseph amesema wamelazimika kuita wananchi ili kuutambua mwili wa marehemu.

Amesema licha ya kiwiliwili kutelekezwa kwenye eneo la kichaka, kichwa cha marehemu huyo wa kiume hakikuwapo kwenye eneo hilo jambo ambalo alilosema limeleta hofu kwa wananchi.

“Nimeita watu na walikusanyika, hata hivyo walishindwa kuubaini mwili huo kwa kuwa kichwa chake hakikuonekana. Mwenyekiti wa Kijiji cha Rushwa alitoa taarifa polisi kwa ajili ya hatua zaidi ili turuhusiwe kuzika,” amesema Joseph

No comments

Powered by Blogger.