Mtu mmoja amefariki dunia kwa kukatwa kichwa na kiwiliwili chake
kutelekezwa kichakani katika Kijiji cha Rushwa, Kata ya Mushabago,
Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Buyango, Gasper Joseph amesema wamelazimika kuita wananchi ili kuutambua mwili wa marehemu.
Amesema licha ya kiwiliwili kutelekezwa kwenye eneo la kichaka, kichwa
cha marehemu huyo wa kiume hakikuwapo kwenye eneo hilo jambo ambalo
alilosema limeleta hofu kwa wananchi.
“Nimeita watu na walikusanyika, hata hivyo walishindwa kuubaini mwili
huo kwa kuwa kichwa chake hakikuonekana. Mwenyekiti wa Kijiji cha Rushwa
alitoa taarifa polisi kwa ajili ya hatua zaidi ili turuhusiwe kuzika,”
amesema Joseph
Post a Comment