Header Ads

MH. LOWASA AITAMANI 2020,AWATAKA VIJANA KUANZA KUJIPANGA NA URAIS 2020

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Democrasia na Maendeleo CHADEMA ambaye pia ni waziri mkuu mstaafu Mh. Edward Lowassa amelitaka baraza la vijana la CHADEMA Taifa kutokukubali kugawanywa katika misingi ya kisiasa na badala yake wajikite katika kukiimarisha chama hicho katika ngazi ya chini hasa vijijini.
Waziri huyo mkuu mstaafu ambaye pia ni mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA Taifa  Mh Edward Lowassa ametoa rai hiyo kwa vijana wakati wa ufunguzi wa mkutanao mkuu wa kamati tendaji ya BAVICHA Taifa na ambapo amehimiza umoja ndani ya baraza hilo na kuwataka kuelekeza nguvu zao mwaka 2020, huku pia akiendelea kusikitishwa na kauli tata za katazo la mikutano ya kisiasa.

John Mrema na Bw. Patrobas Katambi ambaye ni mwenyekiti wa baraza hilo pamoja na masuala mengine wamewataka vijana kuwa mstari wa mbele kuhakikisha demokrasia inapatikana huku pia adhima yao ya  kuelekea mjini dodoma wakisema iko pale pale.

Kikao hicho cha kamati kuu tendaji ya BAVICHA Taifa kilihudhuliwa na wajumbe kutoka mikoa yote Tanzania ambapo pia kinaratajia kutoka na azimio la njia mbadala ya kile inachokiita ni kwenda kulisaidia jeshi la polisi mkoani Dodoma

No comments

Powered by Blogger.