Header Ads

DEMBA BA' AMSAMEHE ALIEMVUNJA MGUU


Lilikuwa ni tukio la kusikitisha pale mshambuliaji nyota wa zamani wa Newcastle na Chelsea Demba Ba alipovunjia mguu akiwa uwanjani kutekeleza majukumu yake.

Jina la Ba limekuwa kwenye vyombo vya habari baada ya kuvunjika mkuu wake wakati wa mchezo wa Shanghai derby.

Akicheza dhidi ya Shanghai SIPG, striker huyo wa Shanghai Shenhua alishuhudia mwish wake wa msimu pale mguu wake wa kulia ulipopinda mithili ya plastic laini.

Siku ya Jumanne, Sun Xiang alimtembelea Demba Ba hospitali ambapo pia Ba alizungumza na vyombo vya habari kwa mara ya kwanza tangu alipoumia.

Demba Ba: Nimefurahi timu imeshinda

Akizungumza na kituo cha television cha Chinese TV, Demba Ba alisema: “Ilikuwa ni siku ngumu (Jumapili) kwa upande wangu na timu nzima, lakini ninafurahi tulishinda.”

“Napenda kuwashukuru mashabiki wote ambao wanakuja kunijulia hali hospitalini.”

Imeripotiwa pia na vymbo vya habari vya China kwamba, Demba Ba amemsamehe Sun Xiang kwa kusema: “Msimlaumu, mimi naendelea vizuri.”

No comments

Powered by Blogger.