Header Ads

MFUNGWA MKONGWE DUNIANI AACHIWA HURU.

Mwanamke mmoja raia wa Bangladesh ambaye anakisiwa kuwa ndiye mfungwa mkongwe zaidi ameachiwa huru.

Ohidunessa mwenye umri wa miaka 100 alihukumiwa kifungo cha maisha jela kimakosa kwa mauaji ya mwanafamilia wake yapata miaka 20 iliyopita.

Bi kizee huyo hata hivyo alipata afueni baada ya jaji mkuu wa nchi hiyo Surendra Kumar Sinha, kuingilia kati.
Image caption Ohidunessa mwenye umri wa miaka 100 alihukumiwa kifungo cha maisha jela kimakosa
Bibi huyo alifaulu kuishawishi mahakama ya rufaa kumuachilia.

Ohidunessa kwa sasa haoni kwa hivyo anahitaji msaada kutekeleza majukumu yake ya kila siku.

Kufikia sasa ametumikia miaka 20 ya kifungo chake cha maiasha

No comments

Powered by Blogger.