NEWS:WANAFUNZI WAHUKUMIWA KIFUNGO BURUNDI KWAK.......(SOMA ZAIDI)
Jeshi la wananchi nchini burundi limewashikilia kundi kubwa la wanafunzi wa chuo kukuu ambao wamekiuka sheria za nchi hiyo kwa kudiriki kumtukana na kuchafua picha za raisi wa nchi hiyo nkurunzinza Wakazi mjini Bujumbura wanasema, watu wawili wamejeruhiwa siku ya
Ijumaa pindi polisi walipopiga risasi kutawanya wanafunzi waliokuwa
wakiandamana.
Waangalizi wanasema maafisa wa serikali walianza kupambana na kile kinachoonekana kuongezeka kwa visa vya kuharibu picha ya rais katika vitabu vya wanafunzi shuleni.
Makundi ya vijana yamehojiwa kutokana na matukio hayo na idadi kubwa inakabiliwa na mashtaka.
Mamia ya wanafunzi, wengine wakiwa na umri mdogo wa miaka kumi na
miwili wamefanya maandamano kutokana na kamatakamata hiyo, lakini
wanasema polisi wamefyatulia risasi.
Mwezi uliopita, zaidi ya wanafunzi mia tatu walitimuliwa shuleni katika mji wa Ruziba baada ya walimu kukuta vitabu vyenye picha ya rais vimeharibiwa kuandikwa ujumbe wa matusi.
Shirika la Umoja wa mataifa linaloshughulikiwa masuala ya watoto UNICEF limelaani kukamatwa na kufukuzwa kwa watotot hao, na kusema shule zinatakiwa kuheshimiwa kama maeneo
salama kwa watoto.
Kumekuwa na hali ya wasiwasi nchini Burundi tangu rais Nkurunziza kuamua kuwania muhula wa tatu kinyume cha katiba ya nchi hiyo hapo mnamo mwaka jana
Waangalizi wanasema maafisa wa serikali walianza kupambana na kile kinachoonekana kuongezeka kwa visa vya kuharibu picha ya rais katika vitabu vya wanafunzi shuleni.
Makundi ya vijana yamehojiwa kutokana na matukio hayo na idadi kubwa inakabiliwa na mashtaka.
Mwezi uliopita, zaidi ya wanafunzi mia tatu walitimuliwa shuleni katika mji wa Ruziba baada ya walimu kukuta vitabu vyenye picha ya rais vimeharibiwa kuandikwa ujumbe wa matusi.
Shirika la Umoja wa mataifa linaloshughulikiwa masuala ya watoto UNICEF limelaani kukamatwa na kufukuzwa kwa watotot hao, na kusema shule zinatakiwa kuheshimiwa kama maeneo
salama kwa watoto.
Kumekuwa na hali ya wasiwasi nchini Burundi tangu rais Nkurunziza kuamua kuwania muhula wa tatu kinyume cha katiba ya nchi hiyo hapo mnamo mwaka jana
Post a Comment