Kiongozi
wa zamani wa Bongo Movie Unit, Steve Nyerere amempongeza msanii wa
muziki, Harmonize pamoja na dancer wa Diamond, Mosei Iyobo kwa kuwapa
utulivu wasanii wenzake wa filamu Aunt Ezekiel na Jacqueline wolper.
Muigizaji huyo ambaye alikuwa MC katika iftar ya GSM iliyofanyika
Kigamboni weekend hii na kuhudhuriwa na mastaa mbalimbali, alisema
anawashukuru wasanii hao wa muziki kwa uwamuzi wa kuwahifadhi dada zake
hao.
“Mimi nashukuru wasanii wa bongofleva kwa kuwahifadhi dada zetu, Aunt
yupo poa, na Wolper naona safi,” alisema Steve Nyerere huku akicheka.
Wolper na Harmonize kwa sasa ni wapenzi na kila mmoja anaonyesha
anampenda mwenzake, na Aunt Ezekiel na Mose Iyobo ni wapenzi wa muda
mrefu na wanaishi kama familia na mtoto wao mmoja aitwae Cookie.
Post a Comment