Watu watatu wamefariki dunia baada ya kula mihogo inayodhaniwa kuwa na sumu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei amesema jana kuwa tukio
hilo juzi saa tisa mchana katika Kijiji cha Kauzeni, Manispaa ya
Morogoro.
Amesema watu hao ni kati ya watano waliokula mihogo hiyo, lakini wawili
walinusurika baada ya kuwahishwa Hospitali ya Jeshi la Wananchi wa
Tanzania (JWTZ) Mzinga kwa matibabu.
Post a Comment