Kiongozi wa wasafi classic amewaambia baadhi ya mashabiki wa Diamond platnumz Mmoja kati ya viongozi wa juu wa label ya ‘WCB’, Babu Tale amesema watu
hawajui kama Ali Kiba na Diamond wakikutana wanazungumza kama kawaida.
dd
Amesema hayo baada ya weekend hii kuzagaa picha katika mitandao ya
kijamii inayomuonyesha Babu Tale, Sallam, Ommy Dimpoz, Mwana FA pamoja
Ali Kiba wote wakiwa na nyuso za furaha hali ambayo liibua maswali mengi
kwa mashabiki.
Akiongea katika kipindi cha XXL cha Clouds Fm, Jumanne hii, Babu Tale
amewataka mashabiki wa muziki kuamiani kwamba yeye pamoja na Diamond
hawana tatizo na Ali Kiba.
“Unajua binadamu wanatakiwa kubadilika, huwezi ukatengeneza dhana sisi
tuna matatizo hatuwezi hata kupiga picha, hatuwezi kukaa pamoja,
hatujafikia hatua hiyo, sisi tunabishana kimuziki na tunatengeneza value
ya muziki ili muziki wa Tanzania ukue,” alisema Tale.
Aliongeza, “Haimaanishi Diamond na Ali Kiba wakikaa hawaongei, watu
hawajui kuna picha ambazo sisi tunazo Diamond na Kiba wanaongea wapo
studio kabisa. Hata kama tukiamua kizipost hizo watu wangeanza
kuzungumza zitu vingine, picha ni kitu cha kawaida. Katika hii picha
ambayo inazungumziwa alianza kuitwa Mwana FA, akaitwa Omary, akaitwa
Ali, tukaitwa mimi na Sallam, kama ningekuwa sitaki kukaa karibu na Kiba
ningekimbilia moja kwa moja kwa na Sallam kwa sababu sisi ni wamwisho
kuitwa,”
Diamond na Ali Kiba ni wasanii ambao wanadaiwa hawaelewani kitu ambacho kimekuwa kikikanushwa na pande zote mbili.
Post a Comment