Msanii
Peter Msechu amefunguka na kusema kuwa yeye mwili wake umemshinda sasa
maana amejaribu kila mbinu kupunguza lakini wapi upo pale pale na yeye
mambo ya kusema afanye diet hawezi kwani hela ya kununu matunda ya elfu
nne kila siku hana.
Peter Msechu amesema hayo kupitia kipindi cha Planet Bongo cha East
Africa Radio na kusema sasa amegundua kitu pekee kinachoweza kupunguza
mwili wake si kufanya diet bali ni kupata stress tu, hivyo anatafuta mtu
wa kumpa stress ili apungue.
"Mambo ya kusema nafanya diet mimi siwezi hizo hela za kununua matunda
ya elfu nne kila siku mimi sina, sijui hela ya gym hamna, saizi mimi
nataka stress tu ili nipungue maana kitambi hiki saizi kimekuwa na
mazalia kama arobaini hivi" alisema Peter Msechu
Mbali na hilo Peter Msechu alisema kuwa katika wimbo wao mpya ambao
wamefanya na Banana Zoro kwa asilimia kubwa umeandaliwa na Banana Zoro
na kusema yeye yupo karibu na Banana Zoro kutokana na ukweli kwamba
wanafanya muziki wa aina moja wa live, na kusema huo ndiyo muziki wa
kweli na si muziki wa wasanii wengi wa bongo ambao wanabebwa bebwa na
computer kwa kutengenezwa.
Post a Comment