NEWS:DIAMOND PLATNUMZ AMPA MAKONDA ZAWADI MAALUMU KAMA ASANTE YA.......(SOMA ZAIDI)
Msanii maarufu tanzania abdul naseeb raisi wa wasafi tanzania ametembelea kwa mkuu wa mkoa wa dar es salaam akiwa na tim yake ya wcb wasafi classic amempelekea mkuu wa
mkoa poul makonda zawadi ya madawati ikiwa ni jumla ya madawati 600 ,diamondi hakudhuru ofisini hapo peke yake amekuja na timu yake yote akiwepo msanii mpya aliesajiliwa hivi karibuni katika kikundi hicho. Msemaji mkuu wa diamond babu tale amesema wamefanya hivyo ikiwa ni njia ya kusaidia wanafunzi ambao bado wanasota na uhaba wa viti mashuleni....
PICHA ZAIDI
Ni June 6, 2016 ambapo staa Diamond Platnumz aliungana na uongozi wake wa label ya WCB kuelekea ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Akizungumza na waandishi wa habari RC Paul Makonda alisema….’Diamond
na uongozi wake wamekuja ofisini kutoa shukrani na pia kuomba niwe kama
mlezi wao wa WCB nitahusika kuwashauri na kuwaelekeza yale watakayotaka
niwashauri katika kazi zao‘-Paul Makonda
‘WCB ni label ambayo ndani yake
kuna vijana wanaofanya kazi zao za sanaa lakini wakiwa na malengo
yakuwekeza kwenye miradi mbalimbali ili kuboresha maisha yao kuongeza
pia pato la uchumi wa taifa letu, sasa kwa kifupi wametoa mchango ambao
unasaidia katika sekta nzima ya Elimu ambapo wametoa madawati 600
tutayapata kutoka kwao ni sehemu yao kusema asante kwa watanzania’– Paul Makonda
Hizi ni baadhi ya picha kutoka kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Post a Comment