Mtu mmoja mkazi wa Kijiji cha Kandashi, wilayani Siha, mkoani
Kilimanjaro, Abedi Akyo (53), amefariki dunia baada ya kudaiwa kuchapwa
viboko na wazee wa kimila kwa tuhuma ya kujihusisha na wizi wa kuku.
Akielezea mazingira ya kifo hicho, Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Kilimanjaro, Wilfred Mutafungwa amedai kuwa Akyo alichapwa viboko 70 na
wazee hao wa kimila wa Kimeru na Kimasai.
Mutafungwa amesema watuhumiwa watafikishwa mahakamani baada ya kuwasiliana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Mwezi uliopita wakazi wa Kata ya Karansi wilayani hapa walitoa uamuzi
kuwa wanawake watakaovaa sketi fupi na vijana watakaovalia suruali chini
ya kiuno, wataadhibiwa kwa kuchapwa viboko 60 hadi 70.
Post a Comment