Header Ads

NEWS; UKIMWI SASA KUPIMWA NYUMBA HADI NYUMBA KWA KUW........(SOMA ZAIDI)

Gazeti la JamboLEO limeripoti kuwa Serikali inakusudia kufanya utafiti kwa kupima virusi vya UKIMWI (VVU) nyumba kwa nyumba kuanzia ngazi ya kaya, ili kupata takwimu sahihi kuhusu hali ya maambukizi mapya ya ugojwa huo ulivyo sasa nchini.

Aidha gazeti hilo limeongeza kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk Albina Chuwa ambapo alisema utafiti huo utakaotumia teknolojia ya kisasa, unalenga kupima viashiria na matokeo ya UKIMWI nchini, ili kujua ni kiwango gani Tanzania imepiga hatua katika kupamban na ugonjwa huo.

Gazeti hilo limemnukuu Dk Albina Chuwa akisema

”utafiti huo utafanyika kwa kutumia sampuli wakilishi ya kaya takribani 15, 800 za Tanzania Bara na Zanzibar kwa kufikia walengwa 40, 000 wakiwamo watoto wasiopungua 8, 000′

No comments

Powered by Blogger.