Header Ads

OFISI ZA BUNGE KUHAMIA DODOMA SEPTEMBER MWAKA HUU.

Ofisi za Bunge zilizopo Jijini Dar es salaam zinatarajia kuhamishiwa Dodoma mwezi Septemba mwaka huu, ikiwa ni utekelezaji wa agiza la Rais Magufuli la kuhamishia shughuli za serikali Dodoma.

Taarifa hiyo imetolewa na Spika wa Bunge, Job Ndugai jana na kusema kuwa kwa bunge suala la luhamia Dodoma siyo gumu kwa kuwa tayari makao makuu yake yako Dodoma.

Alisema tayari alikwishatoa maagizo kwa ofisi yake kuhakikisha kuwa kufikia mwezi Septemba kila kitu kinachofanyika Dar es salaam kifanyike Dodoma isipokuwa mambo  machache.

"Nimeagiza ofisi yangu ihamie dodoma mara moja kuanzia Septemba hii, watumishi wa bunge karibu wote watahamia Dodoma, masuala ya malipo yataangaliwa baadaye, kwa sasa ni kuhamia dodoma tu, ofisi tunazo huko" Alisema Ndugai

Kama sehemu ya mwanzo wa utekelezaji wa azma hiyo, tayari ofisi ya bunge imetangaza kufanyia Dodoma vikao vyake vyote vya kamati za bunge tofauti na ilivyokuwa umepangwa mwanzo na ilivyozoeleka kufanyikia Dar es salaam.

No comments

Powered by Blogger.