Header Ads

BRAZIL YAICHAPA COLOMBIA YATINGA NUSU FINAL OLYMPIC

Timu ya soka ya wanaume ya Brazil, imeingia nusu fainali ya michuano ya Olimpiki baada ya kuwachapa Colombia, 2-0.

Goli la kwanza lilifungwa na mchezaji wa Barcelona, Neymar baada ya kupiga free-kick dakika 12 tu baada ya mchezo kuanza na Luan kuongeza la pili kipindi cha pili.

Brazil sasa itakipiga na Honduras Jumatano kwenye nusu fainali baada ya kuwachapa Korea Kusini, 1-0. Ujerumani itavana na Nigeria waliowafunga Denmark 2-0 na Ujerumani kuwafunga Ureno 4-0.

No comments

Powered by Blogger.