Header Ads

HARMONIZE AKANA KUCHUNWA PESA NA MPENZI WAKE.....




Mwanamuziki wa Bongo Flava anayesimamiwa na Wasafi, Harmonize, amekanusha kuchunwa pesa na mpenzi wake Jackline Wolper kutokana na mwanamke huyo kuonekana kuwa na maisha ya kifahari.

Harmonize amekanusha hayo kwa kusema “Nyumbani kwa Wolper kuna kaunta ambayo anaweza kunywa vinywaji atakavyo, pia sioni sababu ya mimi kupendeza na mwanamke wangu asipendeleze ni lazima nitahakikisha anapendeza kwa kuwa ninampenda”.

Harmonize pia alizidi kuweka wazi kuwa mapenzi yake na Wolper hajaathiri kitu chochote kwenye kusaidia familia ya kwao kwa kuwa hata kama asingekuwa na Wolper ni lazima angekuwa kwenye mahusiano.







“Siyo kwamba ninatumia pesa nyingi kumridhisha mpenzi wangu na kusahau familia yangu, Mama yangu na ndugu zangu wanapata pesa za matumizi kama kawaida kwa kuwa ninafanya kazi”.alisema Hrmonize.

No comments

Powered by Blogger.