Header Ads

KASIM MGANGA,TIP TOP WANANIKWAMISHA KIAINA

Msanii Kassim Mganga ambaye awali alikuwa ni moja kati ya wasanii kutoka katika kundi la Tip Top Connection amesema ukimya wa kundi hilo unamuumiza na kumgusa sababu yeye bado ni mwanafamilia wa Tip Top Connection licha ya kutofautiana kibiashara.

Kassim Mganga akiwa kwenye kipindi cha Planet Bongo alisema yeye bado ni mwanafamilia wa Tip Top Connection hivyo alikuwa anapenda kuona familia yake hiyo inaendelea na moto ule ule kama zamani.

“Unajua unapoongelea Tip Top Connection na Kassim Mganga ni kama familia, hivyo ile ni familia yangu japo tulipishana kwenye masuala ya biashara tu. Hivyo kama mwanafamilia wa Tip Top Connection ukimya wao unanigusa na kuniumiza sababu nilikuwa natamani kuona chama linaendelea na moto ule ule kama zamani” alisema Kassim Mganga

Mbali na hilo Kassim Mganga ameahidi kuja na band yake katika siku zijazo kwani anatamani kufanya muziki wa live kwenye show zake.

No comments

Powered by Blogger.