KASIM MGANGA,TIP TOP WANANIKWAMISHA KIAINA
Kassim Mganga akiwa kwenye kipindi cha Planet Bongo alisema yeye bado ni mwanafamilia wa Tip Top Connection hivyo alikuwa anapenda kuona familia yake hiyo inaendelea na moto ule ule kama zamani.
“Unajua unapoongelea Tip Top Connection na Kassim Mganga ni kama familia, hivyo ile ni familia yangu japo tulipishana kwenye masuala ya biashara tu. Hivyo kama mwanafamilia wa Tip Top Connection ukimya wao unanigusa na kuniumiza sababu nilikuwa natamani kuona chama linaendelea na moto ule ule kama zamani” alisema Kassim Mganga
Mbali na hilo Kassim Mganga ameahidi kuja na band yake katika siku zijazo kwani anatamani kufanya muziki wa live kwenye show zake.
Post a Comment