NEWS:RAISI SHEIN ATEUWA WAKUU WA MIKOA ZANZIBAR ......(SOMA ZAIDI)
Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na
Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar imesema walioteuliwa ni Mkuu wa Mkoa wa
Mjini na Magharibi ambaye anakuwa Ayoub Mohamed Mahmoud na Mkuu wa Mkoa
wa Kaskazini, Unguja Vuai Mwinyi Mohamed.
Taarifa hiyo imesema Wakuu wa Mikoa ambao Mikoa yao haikutajwa katika taarifa hii wanaendelea na dhamana zao kama kawaida.
Halikadhalika Rais Shein amemteua Marina Joel Thomas kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Silima Haji Haji kuwa Mkuu wa Wilaya ya Magharibi B, Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini A anakuwa Hassan Ali Kombo, Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B anakuwa Issa Juma Ali, Mkuu wa Wilaya ya Kati Mashavu Sukwa Said, Mkuu wa Wilaya ya Kusini Idrissa Kitwana Mustafa na Mkuu wa Wilaya ya Chakechake Salama Mbarouk Khatib.
Aidha Wakuu wa Wilaya ambao Wilaya zao hazikutajwa katika taarifa hii wanaendelea na dhamana zao kama kawaida.
Uteuzi wa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya umeanza leo.
Viongozi wote walioteuliwa wanatakiwa waripoti Ikulu, Mjini Unguja, siku ya Jumanne tarehe 24 Mei 2016 mchana tayari kwa kuapishwa.
Taarifa hiyo imesema Wakuu wa Mikoa ambao Mikoa yao haikutajwa katika taarifa hii wanaendelea na dhamana zao kama kawaida.
Halikadhalika Rais Shein amemteua Marina Joel Thomas kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Silima Haji Haji kuwa Mkuu wa Wilaya ya Magharibi B, Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini A anakuwa Hassan Ali Kombo, Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B anakuwa Issa Juma Ali, Mkuu wa Wilaya ya Kati Mashavu Sukwa Said, Mkuu wa Wilaya ya Kusini Idrissa Kitwana Mustafa na Mkuu wa Wilaya ya Chakechake Salama Mbarouk Khatib.
Aidha Wakuu wa Wilaya ambao Wilaya zao hazikutajwa katika taarifa hii wanaendelea na dhamana zao kama kawaida.
Uteuzi wa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya umeanza leo.
Viongozi wote walioteuliwa wanatakiwa waripoti Ikulu, Mjini Unguja, siku ya Jumanne tarehe 24 Mei 2016 mchana tayari kwa kuapishwa.
Post a Comment