NEW::TAMBWE ABAINISHA SIRI YA MAFANIKIO(UBINGWA) KWENY..........(SOMA ZAIDI)
Mshambuliaji anaeongoza kufunga magoli mengi
kwenye ligi kuu Tanzania Bara Amis Tambwe amesema kutulia mbele ya lango
na kuwa na malengo ndio kunakomfanya mara nyingi aibuke kuwa mfungaji
bora
Tambwe abainisha siri ya mafanikio
Mshambuliaji huyo toka Burundi ameiambia TBC kuwa mara
nyingi kabla ya kuanza kwa ligi anakuwa na malengo ya kufunga magoli
mengi pia aliwahi kupata mafunzo ya jinsi ya kufunga magoli wakati akiwa
mdogo.Hadi sasa Tambwe ameshafunga magoli 21 akiwa mbele ya mshambuliaji wa Simba, Hamis Kiiza mwenye magoli 19 na kama atafanikiwa kuibuka kuwa mfungaji bora msimu huu basi hii itakuwa ni mara yake ya pili kufanya hivyo.
Katika hatua nyingine Tambwe amempongeza Donald Ngoma mshambuliaji anaeshirikiana nae kwenye timu hiyo na kusema amechangia yeye kufunga magoli hayo.
Post a Comment