Header Ads

NEWS:: RAIS MAGUFULI ATEUA MAKATIBU TAWALA WA MIKOA 26...(SOMA ZAIDI)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Aprili, 2016 amefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara.

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa kati ya Makatibu tawala hao 10 ni wapya, 2 wamebadilishiwa vituo vya kazi na 13 wamebakisha katika vituo vyao vya sasa.

Makatibu Tawala wapya walioteuliwa ni kama ifuatavyo;

  1. Arusha - Richard Kwitega
  2. Selestine Muhochi Gesimba - Geita
  3. Armatus C. Msole - Kagera
  4. Eng. Aisha Amour - Kilimanjaro
  5. Zuberi Mhina Samataba - Pwani
  6. Albert Gabriel Msovela - Shinyanga
  7. Dr. Angelina Mageni Lutambi - Singida
  8. Jumanne Abdallah Sagini - Simiyu
  9. Dkt. Thea Medard Ntara - Tabora
  10. Eng. Zena Said - Tanga
Makatibu Tawala waliobadilishwa vituo vya kazi ni kama ifuatavyo;
  1. Kigoma - Charles Amos Pallangyo (Kutoka Mkoa wa Geita)
  2. Morogoro - Dkt. John S. Ndunguru (Kutoka Mkoa wa Kigoma)
Makatibu Tawala waliobakishwa katika vituo vyao vya sasa vya kazi ni kama ifuatavyo;
  1. Dar es salaam - Theresia Louis Mbando
  2. Dodoma - Rehema Hussein Madenge
  3. Iringa - Wamoja Ayubu Dickolagwa
  4. Katavi - CP Paul Chagonja
  5. Lindi - Ramadhan Habibu Kaswa
  6. Mara - Benedict Richard Ole Kuyan
  7. Manyara - Eliakimu Chacha Maswi
  8. Mbeya- Mariam Amri Mjunguja
  9. Mtwara - Alfred Cosmas Luanda
  10. Mwanza - CP. Clodwing Mathew Mtweve
  11. Njombe - Jackson Lesika Saitabau
  12. Rukwa - Symthies Emmanuel Pangisa
  13. Ruvuma - Hassan Mpali Bendeyeko
Makatibu Tawala wa Mikoa 10 ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza, wataapishwa siku ya Jumatano tarehe 27 Aprili, 2016 saa tatu asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
25 Aprili, 2016

No comments

Powered by Blogger.